Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Sugu achomoka kwa dhamana, kutinga polisi leo
Habari Mchanganyiko

Sugu achomoka kwa dhamana, kutinga polisi leo

Spread the love

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu)-Chadema jana jioni alifanikiwa kupata dhamana baada ya kukamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Mbeya asubuhi ya siku hiyo kwa madai ya uchochezi. Anaripoti Bupe Mwakiteleko … (endelea).

Sugu alifika kituoni hapa jana asubuhi akiitikia wito wa jeshi hilo uliomtaka kufanyi hivyo kwa madai ya kukashifu mamlaka za serikali hususani kukejeli ugawaji wa vitambulisho vya mjasiriamali.

Mbunge huyo alipifika kwenye Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya kwa ajili ya kuhojiwa kuhusu video unayosambaa akionekana ‘kukejeli’ mamlaka za serikali, alizuiwa kutoka.

Sugu anadaiwa kutoa kauli hiyo alipozungumza na wananchi wakati akitoa msaada katika Shule ya Msingi Ikuti, Mbeya. Hata hivyo, Jeshi la Polisi mkoani humo lilimpa dhamana majira ya saa 1 jioni baada ya kuwekewa dhamana ya bondi ya Sh 5 milioni. L anatakiwa kwenda kuripoti kituoni hapo.

Urich Matei, Makanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya amesema, kuwa kesi ya Sugu ni ya uchochezi na kwamba, amepewa dhamana huku uchunguzi ukiendela.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Makamba: China ni ya mfani kwa kupunguza umaskini

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, January...

error: Content is protected !!