Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Stars yakaa kileleni kundi J
HabariMichezo

Stars yakaa kileleni kundi J

Spread the love

TIMU ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imerejea tena kwenye usukani wa kundi J, katika harakati za kutafuta tiketi za kufuvu fainali za kombe la Dunia zitakazofanyika Qatar 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Mabadiliko hayo yamekuja mara baada hii leo tarehe 10 Oktoba 2021, kupigwa michezo miwili kwenye kundi hilo kwa mzunguko wa pili.

Katika mchezo wa kwanza uliofanya Stars kufufua matumaini, walifanikiwa kuondoka na ushindi wa bao 1-0, wakiwa ugenini dhidi ya Benin.

Bao hilo pekee la Tanzania kwenye mchezo huo, lilifungwa na mshambuliaji Simon Msuva kwa shuti kali kwenye dakika ya 6.

Matokeo hayo yaliwafanya Stars, kufikisha pointi saba, sawa na Benin lakini kukiwa na utofauti wa mabao yakufungwa na kushinda.

Mchezo wa pili uliofuta uliwakutanisha Madagascar ambao walikuwa nyumbani dhidi ya Jamhuri ya Congo, na wenyeji hao kufanikiwa kuondoka na ushindi wa bao 1-0.

Kipigo hiko kiliwafanya Congo kusalia na pointi zaao 5, kwenye nafasi ya tatu, huku Madagascar akiendelea kuburuza mkia akiwa na alama tatu, ukiwa ndio mchezo wao wa kwanza kushinda.

Kundi hilo sasa limebakisha michezo miwili kwa kila timu, ambayo itapigwa tarehe 11 na 14, Novemba 2021, ambapo Stars itaanza kushika Dimbani nyumbani dhidi ya Jamhuri ya Congo, na baadae wataenda ugenini kwenye mchezo wa mwisho dhidi ya Madagascar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!