Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Standard Chartered yatoa Bil 1.5 kuchenga reli
Habari za Siasa

Standard Chartered yatoa Bil 1.5 kuchenga reli

Spread the love

TANZANIA kupata mkopo nafuu wa dola za Marekani bilioni 1.46 sawa na zaidi ya shilingi trilioni 3.3 kutoka kwa Benki ya Standard Chartered Group kwa ajili ya kujenga kipande cha Reli ya Kiwango cha Kimataifa (SGR) kuanzia Morogoro hadi Makutupora, mkoani Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hayo yameelezwa na Dk. Philip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Bill Winters Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Jijini Dar es Salaam.

“Tunajenga Reli hiyo ya Kisasa kutoka Dar es Salaam – Morogoro hadi Makutupora ambazo ni awamu mbili lakini pia tutajenga reli hiyo kuelekea Isaka mpaka Mwanza na baadaye Rusumo ambapo wenzetu wa nchi ya Rwanda, tutasaidiana, wao watajenga reli hiyo kutoka Rusumo hadi Kigali” Aliongeza Dk. Mpango.

Dkt. Mpango ameishukuru Benki hiyo kwa kukubali kugharamia ujenzi wa Reli hiyo ya kisasa ambayo lengo lake ni kuimarisha usafiri na usafirishaji wa abiria na mizigo kwenda bara na nchi jirani za Maziwa Makuu na zile ambazo hazipakani na Bahari.

Naye Bill Winters, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered Group, ameipongeza Tanzania kwa kupiga hatua kubwa kiuchumi na kwamba Benki yake itatoa mkopo huo na kuahidi kuwa balozi wa kuelezea mafanikio makubwa ya kiuchumi ya Tanzania kwa wadau wengine.

Katika kikao hicho, Bw. Bill Winters aliambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo nchini Kenya na nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki Bw. Lamin Manjang na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo nchini Tanzania Bw. Sanjay Rughani, ambapo pia Benki hiyo inafanya shughuli zake hapa nchini kwa kipindi cha miaka 101 sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!