Saturday , 2 December 2023
Home Kitengo Biashara Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu
BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the love

SHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu wenye ulemavu nchini kupitia fursa ya uwakala na uuzaji wa mkaa mbadala wa Rafiki briquettes.

Mkaa huo ambao ni rafiki wa mazingira unasaidia kuunga mkono juhudi za serikali kukabilina na mabadiliko tabianchi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma… (endelea)

Mkurugenzi wa Shirika la Foundation For Disabilities Hope (FDH), Michael Salali, amebainisha hayo leo tarehe 27 Septemba 2023 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu fursa hiyo.

Amesema shirika la STAMICO, limeanzisha utengenezaji wa mkaa mbadala ambao unafahamika kwa jina la Rafiki briquettes, ambapo watu wenye ulemavu watapatiwa fursa ya kuwa mawakala na wauzaji wa bidhaa hiyo.

“Tunalishukuru sana shirika la STAMICO kwa fursa hii kwa watu wenye ulemavu ambayo inakwenda kusaidia kuwakwamua kiuchumi.

“Kama mnavyofahamu watu wenye ulemavu nchini uchumi wao bado ni duni sana hivyo fursa hii itasaidia kuboresha maisha yao na kuwaondolea changamoto ya unyanyapaa wanaokumbana nao katika jamii zao”amesema

Pia, amesema mkaa huo mbadala utasaidia kuendeleza juhudi za serikali na dunia kwa ujumla katika kukabilina na tatizo la mabadiliko tabia ya nchi yatokanayo na uharibifu wa mazingira kwa kukataji miti hovyo.

“Kama mnavyofahamu dunia ipo katika mapambano dhidi ya mabadiliko tabia nchi lakini pia uharibifu mazingira ambao unachangia watu wenye ulemavu wa ngozi kupata saratani ya ngozi kutokana na mionzi ya jua inayosababishwa na ukosefu wa vimvuli… yote hayo yanatokana na ukataji miti kiholela unaendelea nchini” amesema

Aidha, ametoa wito kwa watu wenye ulemavu nchini kuchangamkia fursa hiyo adhimu ili kujikwamua kichumi na kuacha kuendelea kuwa tegemezi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML waungana na Biteko kuanika mbinu za mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Biashara

Shinda mtonyo mrefu ukicheza Shaolin Crew kasino ya  Meridianbet

Spread the love  TAIFA la Uchina limebebwa na historia kubwa sana, wengi...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mwalimu jela miaka mitatu kwa rushwa

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mfawidhi, wilaya ya Igunga, mkoani Tabora imemhukumu...

Habari Mchanganyiko

Waziri Bashungwa aagiza wahandisi kujengewa uwezo

Spread the loveWAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameiagiza Bodi ya Usajili wa...

error: Content is protected !!