SHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limesaini mkataba na Kampuni ya ABSA yenye makao yake nchini Swiss utakaoliwezesha shirika hilo kuiuzia kampuni hiyo tani 60,000 za makaa ya mawe kila mwezi kwa muda wa miaka mitano. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Hafla hiyo ya utiaji saini mkataba huo imefanyika leo tarehe 10 Mei, 2022 jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Naibu Waziri wa Madini Dk. Steven Kiruswa.
Akizungumza katika hafla hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO, Dk. Venance Mwasse amesema, hatua hiyo ni matokeo ya jitihada na mikakati wa kuanza uchimbaji mkubwa wa makaa ya mawe.
Amesema thamani ya mkataba huo ni zaidi ya dola za Marekani milioni 108 sawa na Sh. bilioni 250 kwa miaka mitano
Aidha, Rais wa Kampuni ya ABSA, Gerges Schmickrath ameishukuru Wizara ya Madini kupitia STAMICO kwa kuaminiwa kuwekeza katika mradi huo wa makaa ya mawe.
Amesema mradi huo utakuwa wa manufaa kwa Watanzania na kuongeza pato la Taifa. Makaa haya ya mawe yanayotoka mkoani Songwe katika mgodi wa Kabulo.
Leave a comment