Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Tulia atoa maagizo serikalini ajira za watumishi wanaojitolea
Habari za Siasa

Spika Tulia atoa maagizo serikalini ajira za watumishi wanaojitolea

Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson
Spread the love

 

SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, ameagiza Serikali kuweka kanzi data maalum (data base), yenye taarifa za watumishi wanaojitolea ili wapewe kipaumbele katika mchakato wa ajira. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Spika Tulia ametoa agizo hilo leo tarehe 6 Aprili 2023, bungeni jijini Dodoma, baada ya Mbunge Viti Maalum, Felista Njau kuhoji lini Serikali itaajiri watalaamu wanaojitolea kwa muda mrefu kufanya kazi katika sehemu mbalimbali nchini.

“Waziri wa Afya na wa TAMISEMI, nafikiri kuna haja ya kukaa na Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, sababu watumishi wa afya wanaojitolea na walimu wanaojitolea huwa haipendezi sana kuachwa kwenye ajira. Sababu ajira zikitangazwa wale wanaojitolea unajikuta kwenye eneo lako hakuna mmoja aliyepata ajira, tunajiuliza hawana sifa na wanaokaa nyumbani ndiyo wana sifa?” amesema Dk. Tulia na kuongeza:

“Nafikiri mtengeneze utaratibu mzuri ili kila mwaka mpate taarifa za wanaojitolea ili ajira zinapopatikana mzitumie taarifa hizo kuwapa kipaumbele.”

Awali akimjibu Njau, Naibu Waziri wa Afya, Dk. Godwin Mollel, alisema wizara imetoa muongozo wa kuwalipa nusu mshahara watumishi wanaojitolea kwa kutumia mapato ya ndani.

Aidha, Dk. Mollel alisema hospitali za mikoa, kanda na taifa zimeweza kuwalipa mishahara kamili asilimia 40 ya watumishi wanaojitolea , kwa kutumia mapato ya ndani.

Alisema Wizara ya Afya, itashirikiana na Wizara Ofisi ya Rais TAMISEMI, kuangalia namna bora ya kuwapa kipaumbele kwenye ajira watumishi wanaojitolea kuliko waliokuwa nje ya mfumo huo wakisubiri ajira moja kwa moja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia atua Uturuki kwa ziara ya siku 5

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano amewasili nchini Uturuki kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

Habari za Siasa

Rais Samia amfariji mjane wa Musa Abdulrahman

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne amempa pole Mwanakheri Mussa...

error: Content is protected !!