Sunday , 3 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai: Bunge halina ugomvi na Ofisi ya CAG
Habari za Siasa

Spika Ndugai: Bunge halina ugomvi na Ofisi ya CAG

Prof. Mussa Assad, Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali. Picha ndogo Job Ndugai, Spika wa Bunge
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge ameeleza kwamba, taasisi anayoiongoza haina ugomvi na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), bali lina ugomvi na mtu (Prof. Mussa Assad). Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Amesema, ameamua kutoa ufafanuzi huo kutokana na redio moja nchini kutoa habari za kupotosha kwamba, Bunge limegoma kufanya kazi na Ofisi ya CAG.

Maswali yamekuwa yakiibuliwa kwamba, ni kwa namna gani Bunge linaweza kufanya kazi na Ofisi ya CAG bila maofisa wa ofisi hiyo kupata maelekezo kutoka kwa mkuu wa taasisi hiyo, Prof. Assad.

Miongoni mwa waliohoji swali hilo ni Askofu Benson Bagonza, Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Karagwe ambaye amehoji; “Bunge limepitisha kutofanya kazi na Prof. Assad au CAG?”

Na kwamba, kama Bunge limegoma kufanya kazi na Prof. Assad ambapo Rais John Magufuli siku chache zijazo atapeleka ripoti ya mkaguzi isomwe bungeni, akiipeleka atakuwa amelidharau Bunge na akiacha atakuwa amevunja katiba.

Hata hivyo, Prof. Assad akizungumza na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) alisema, Bunge linapaswa kupitia uamuzi wake kwa kuwa, unaweza kusababisha mgogoro mkubwa kinyume na inavyoonekana sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko aagiza wakurugenzi TANESCO kukemea rushwa kwenye maeneo yao

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Uongozi wa Samia kuendelea hadi 2030

Spread the loveKWETU sisi tuliowahi kusoma sekondari, iwe O levo au A...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Bado askari wastaafu wanaonewa

Spread the loveRAIS wangu Samia Suluhu Hassan tunaendelea kumshukuru Mungu kwamba wote...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Tunastawisha ufisadi na kuchukia matunda yake

Spread the loveBUNGE la Jamhuri linaloendelea mjini Dodoma, kwa wiki nzima limetawaliwa...

error: Content is protected !!