Monday , 11 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai azipiga stop AZAKI kujihusisha na siasa
Habari za Siasa

Spika Ndugai azipiga stop AZAKI kujihusisha na siasa

Job Ndugai
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge amezitaka Asasi za Kiraia nchini (AZAKI) kufanya shughuli zao walizosajiliwa na kuachana na masuala ya siasa, kwani wenyewe ni wanasiasa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Spika Ndugai ametoa kauli hiyo jana tarehe 8 Novemba 2019, katika hafla ya kufunga wiki ya AZAKI, iliyofanyika jijini Dodoma.

Aidha, Spika Ndugai amezitoa hofu AZAKI kuhusu Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020, kwamba utafanyika kwa amani na utulivu.

“Muendelee kuwa na amani na utulivu, msiwe na wasiwasi tunapoelekea kwenye uchaguzi huo mkuu. Mengine ya wanasiasa mtuachie wenyewe, na wale mnaotaka kuingia kwenye siasa karibuni sana,” amesema Spika Ndugai.

Wakati huo huo, Spika Ndugai amezishukuru AZAKI kwa kutoa ushirikiano mzuri kwa serikali na kwake pia.

“Wana AZAKI mwakani ni mwaka wa uchaguzi uchaguzi  mkuu wa nchi yetu , ambako kutakuwa na uchaguzi wa madiwani, wabunge, lakini pia naamini rais wetu (John Magufuli) ataendelea. Sina hakika kama nitapata nafasi ya kukutana nanyi, kama mtaendelea kufanya maazimisho katika mwezi kama huu,” amesema Spika Ndugai na kuongeza;

“Maana wakati huo tutakuwa kwenye harakati kubwa sana, tarehe kama hizi uchaguzi mkuu ndio unakuwa ushafanyika, wanaokata rufaa wanakimbilia mahakamani, bunge linaundwa anapatikana spika mpya,  baraza jipya la mawaziri, kwa mazingira hayo niwashukuruni sana kwa jinsi ambavyo mmenipa ushirikiano.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Jaji Kiongozi akerwa wananchi kukosa imani na mahakama

Spread the loveWATENDAJI wa Mahakama ya Tanzania, wametakiwa kuweka mikakati itakayosaidia kurejesha...

BurudikaHabari za Siasa

Samia amchangia Professa Jay mil. 50, Chadema, wasanii wamwaga manoti

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amechangia kiasi cha Sh 50 milioni...

Habari za Siasa

Biteko: Samia ni muumini wa maridhiano sio kwa kuigiza

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

error: Content is protected !!