Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai awananga wapinzani
Habari za Siasa

Spika Ndugai awananga wapinzani

Spika wa Bunge, Job Ndugai
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge ametumia ujio wa Mukabalisa Donatile, Spika wa Bunge la Rwanda kuwanaga wapinzani nchini. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Spika Ndugai akizungumza bungeni jijini Dodoma wakati wa kumtambulisha Spika Donatile leo tarehe 10 Juni 2019 amesema, wapinzani wa Rwanda hapingi kila kitu kama walivyo wapinzani wa Tanzania.

Spika Ndugai amesema, Rwanda iko tofauti na Tanzania kutokana na kuwa na vyama vya ushindani na si vya kupinga kila kitu.

“Tofauti na hapa kwetu ni kwamba, Spika wa Rwanda kwenye Katiba yao anatoka chama tofauti na tawala, lakini niseme kwamba Rwanda hawana vyama pinzani vya kupinga kila kitu kama hapa.

“Wao wana vyama ushindani tofauti kubwa ni hapo, kile cha kupinga na kubisha haiwezekani,” amesema Spika Ndugai.

Spika Donatile aliwasilisi nchini jana tarehe 9 Juni 2019 kwa ziara ya kikazi ya siku tatu, ikiwemo kukutana na wabunge, kamati mbalimbali za Bunge, Chama cha Wabunge Wanawake (TGWP).

Pia, atafanya ziara katika maeneo mbalimbali jijini Dodoma na kumtembelea Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!