Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Spika Ndugai asitisha ziara Kamatiza Bunge
HabariTangulizi

Spika Ndugai asitisha ziara Kamatiza Bunge

Spika Job Ndugai
Spread the love

 

KUFUATIA kifo cha Rais wa Tanzania, Dk. John Magufuli, kilichotokea tarehe 17 Machi 2021 katika Hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam, Spika wa Bunge, Job Ndugai amesitisha ziara za kamati za mhimili huo za kukagua miradi mbalimbali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Agizo hilo la Spika Ndugai limetolewa leo Alhamisi tarehe 18 Machi 2021, baada ya kifo cha Rais Magufuli kutangazwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Spika, Spika Ndugai amewaagiza wajumbe wa kamati hizo kurejea mara moja katika Makao Makuu ya Nchi, Dodoma.

“Kufuatia msiba huu mkubwa, Mheshimiwa Spika ameagiza kamati zote za Bunge zilizokuwa katika ziara za ukaguzi wa miradi ya maendeleo mikoani, kurejea Dodoma mara moja,” imesema taarifa ya Ofisi ya Spika.

Wairi Mkuu akihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Akielezea kifo cha Rais Magufuli, Spika Ndugai amesema msiba huo ni mzito ambapo ametoa pole kwa mke wa marehemu, Mama Janeth Magufuli, familia yake, Mama Samia na Watanzania kwa ujumla.

“Tumempoteza Rais wetu kipenzi aliyejitoa kuwatumikia Watanzania wote kwa uadilifu, umahiri, bidii na moyo wa uzalendo wa hali ya juu.

“Kwa niaba ya Bunge, natoa pole kwa Mama Janeth Magufuli na familia ya marehemu, Makamu wa Rais pamoja na Watanzania wote kufuatia msiba huu mzito wa kitaifa,” amesema Spika Ndugai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!