Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Spika Ndugai aota uchaguzi 2025
Habari Mchanganyiko

Spika Ndugai aota uchaguzi 2025

Job Ndugai Spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania
Spread the love

 

SPIKA wa Bunge, Job Ndugai amesema, mwenendo wa utendaji wa Serikali ya Awamu ya Sita, katika kutenga fedha za miradi ya maendeleo, kwamba ifikapo 2025 ‘itachukua na kuweka waah.’ Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Spika Ndugai ametoa kauli hiyo leo Jumanne, tarehe 22 Juni 2021, wakati Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, akifunga mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka wa fedha wa 2021/22, bungeni jijini Dodoma.

Licha ya Spika Ndugai kutotaja tukio mahususi ambalo serikali hiyo inayoongozwa na Chama Cha Mpainduzi (CCM), itakwenda kuchukua na kuweka waah, 2025 Tanzania inatarajiwa kufanya Uchaguzi Mkuu.

“Kwa mtazamo huu naamini tukiendelea hivi katika  miaka miwili mitatu  inayokuja,  2025 basi tena.  Ni kuchukua  na kuweka waah,  hakuna jambo lingine kabisa kabisa,” amesema Spika Ndugai.

Spika Ndugai amesema vyanzo vipya vya mapato vilivyomo katika bajeti ijayo, vitaiingizia  mabilioni ya fedha Serikali, ambayo yatasaidia kutekeleza miradi mbalimbali, ikiwemo ujenzi wa mradi wa ufuaji umeme katika Bwawa la Umeme la Julius Nyerere, kwenye Mto Rufiji na ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR),.

Pia, Spika Ndugai amesema Serikali hiyo iliyoko chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, imefanikiwa kuongeza fedha za utoaji mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania na Mwenyekiti wa Ccm

“Sababu pamoja na bajeti ile tuliyoipitisha,  kwa maamuzi ya kodi, jinsi ambavyo nyongeza ya mabilioni ya fedha yanavyoenda katika maji,  barabara,  makazi,  afya, mikopo ya wanafunzi elimu juu, masuala ya reli,  bwawa la umeme, zile shida za wananchi ambazo wabunge tunahangaika nazo, haijapa kutokea, naipongeza Serikali,” amesema Spika Ndugai.

Mbunge huyo wa Kongwa (CCM), amesema uhitimishwaji mjadala wa bajeti hiyo haujawahi kutokea, hususani mapendekezo mapaya yaliyotolewa na Serikali kupitia tukio hilo.

“Miaka mingi kama mbunge,  kweli kutoka moyoni mwangu sijawahi kuona Serikali ikija na uhitimishaji wa bajeti wa iana hii ya leo.  Sisi kama wabunge tunapaswa kumpongeza  rais wetu kwa mapendekezo haya yaliyokuja leo,” amesema Spika Ndugai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!