Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai amjibu Mbowe
Habari za Siasa

Spika Ndugai amjibu Mbowe

Job Ndugai Spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania
Spread the love

HOTUBA ya Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ‘imemkera’ Spika wa Bunge, Job Ndugai. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Kwa kifupi akijibu kile kilichomo kwenye hotuba ya Mbowe aliyoitia Jumapili ya tarehe 11 Aprili 2021, Spika Ndugai amesema ‘Mbowe anapotosha umma.’

“…sasa huyo rafiki yangu Freeman Mbowe, alikuwa Ulaya huko, sasa katumwa na watu wake huko, anapotosha mambo,” amesema.

Kwenye hotuba yake, pamoja na mambo mengine Mbowe alilituhumu Bunge kwa vitendo vya rushwa.

Hivyo, Spika Ndugai ameagiza Kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC) na ile ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), kufanya uchambuzi wa haraka Ripoti ya Mdhibiti na Mkuguzi wa Hesabu za Serikali (CAG).

Na kwamba, baada ya kufanya uchambuzi huo, uwasilishwe bungeni kwenye mkutano wa nne badala ya mkutano wa tano.

Spika Ndugai amesema, amefanya uamuzi huo kwa kuwa, ripoti hiyo imekuwa ikipotoshwa kwa kiwango kikubwa.

Kiongozi huyo wa bunge amesema, Watanzania wengi hawana uwelewa wa kuchambua taarifa za kihasibu. Kutokana na hivyo, kunaweza kusababisha upotofu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!