Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai amjibu Mbowe
Habari za Siasa

Spika Ndugai amjibu Mbowe

Job Ndugai Spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania
Spread the love

HOTUBA ya Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ‘imemkera’ Spika wa Bunge, Job Ndugai. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Kwa kifupi akijibu kile kilichomo kwenye hotuba ya Mbowe aliyoitia Jumapili ya tarehe 11 Aprili 2021, Spika Ndugai amesema ‘Mbowe anapotosha umma.’

“…sasa huyo rafiki yangu Freeman Mbowe, alikuwa Ulaya huko, sasa katumwa na watu wake huko, anapotosha mambo,” amesema.

Kwenye hotuba yake, pamoja na mambo mengine Mbowe alilituhumu Bunge kwa vitendo vya rushwa.

Hivyo, Spika Ndugai ameagiza Kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC) na ile ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), kufanya uchambuzi wa haraka Ripoti ya Mdhibiti na Mkuguzi wa Hesabu za Serikali (CAG).

Na kwamba, baada ya kufanya uchambuzi huo, uwasilishwe bungeni kwenye mkutano wa nne badala ya mkutano wa tano.

Spika Ndugai amesema, amefanya uamuzi huo kwa kuwa, ripoti hiyo imekuwa ikipotoshwa kwa kiwango kikubwa.

Kiongozi huyo wa bunge amesema, Watanzania wengi hawana uwelewa wa kuchambua taarifa za kihasibu. Kutokana na hivyo, kunaweza kusababisha upotofu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!