Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai aimwagia sifa Kenya
Habari za SiasaKimataifa

Spika Ndugai aimwagia sifa Kenya

Bunge la Kenya
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge ameipongeza Kenya kwa kuzindua Kanuni za Kudumu za Bunge lake, kwa lugha ya Kiswahili. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Spika Ndugai ametoa pongezi hizo leo tarehe 31 Oktoba 2019, wakati akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, nchini Kenya.

Aidha, Spika Ndugai amelipongeza Bunge la Kenya kwa hatua ya kuanzisha utaratibu wa kurusha moja kwa moja, matangazo ya vikao vya kamati mbalimbali.

“Nawapongeza kwa uzinduzi, kwamba sasa vikao vya kamati mbalimbali vitapeperushwa mubashara,” amepongeza Spika Ndugai.

Pia amezitaka nchi za Afrika Mashariki kutumia lugha ya Kiswahili katika vikao vyake vya Bunge.

“Nchi zetu kwa muda mrefu zimefunikwa na kasumba ya kuamini kwamba, lugha zetu ni dhaifu na za watawala wetu ni lugha za juu.

“Hatuna sababu za kuwa wanyonge kwa kutumia kiswahili bungeni,” amesema Spika Ndugai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

error: Content is protected !!