Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Dk. Tulia asema nchi imepiga hatua kidemokrasia
Habari za Siasa

Spika Dk. Tulia asema nchi imepiga hatua kidemokrasia

Spread the love

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Dk. Tulia Ackson, amesema katika kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, nchi imepiga hatua kwenye masuala ya demokrasia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Spika Tulia ametoa kauli hiyo leo Jumamosi, tarehe 19 Machi 2022, akifungua kongamano la tathmini ya mwaka mmoja wa Rais Samia madarakani, lililofanyika kwenye Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), jijini Dodoma.

Spika Tulia amesema, kuimarika kwa demokrasia kunathibitishwa na kitendo cha Mwenyekiti wa Chama cha ADC Taifa, Hamad Rashid, kushiriki kongamano hilo.

“Hapa mmemuona mzee wetu Hamad Rashid, kitendo cha yeye kuwepo hapa kuja kufanya tathmini ya mwaka mmoja wa Rais Samia, kunaashiria kwamba nchi yetu kidemokrasia tumepiga hatua, tunaweza kukaa pamoja namna hii, tukajadiliana pamoja na tofauti zetu za vyama, tunapiga hatua ndani na nje ya nchi,” amesema Spika Tulia.

Aidha, Spika Tulia amesema Rais Samia amefanikiwa kuimarisha demokrasia ya kiuchumi, kwa kufanya ziara katika mataifa ya nje.

“Kwenye eneo la uwekezaji na kukua kwa demokrasia kumesaidia hata demokrasia ya uchumi. Nyie mmeona akizunguka kwenye mataifa mbalimbali kutafuta fursa ambazo zinalifanya Taifa letu lipige hatua. Sasa hatua tunapiga sio tu Taifa letu kwa upande wa maendeleo,” amesema Spika Tulia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!