Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari Spika atoa pongeza kwa Rais Samia uzinduzi wa Royal Tour Marekani
Habari

Spika atoa pongeza kwa Rais Samia uzinduzi wa Royal Tour Marekani

Dk. Tulia Ackson, Spika wa Bunge la Tanzania
Spread the love

 

Spika wa Bunge la Tanzania, Tulia Akson, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kuzindua makala maalumu ya kutangaza vivutio vya utalii nchini inayofahamika kama ‘Royal Tour’ jijini New York, nchini Marekani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Pongezi hizo zimetolewa leo Jumanne, tarehe 19 Aprili 2022, bungeni jijini Dodoma na Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson.

Spika Tulia amesema wabunge wametoa pongezi hizo, kwa kuwa Rais Samia ametekeleza kiu yao ya kuongeza idadi ya watalii.

“Tunatambua siku ya jana Rais Samia Suluhu Hassan, amezindua makala maalumu ya kuhamasisha utalii Tanzania na kwa sababu wabunge huwa mnachangia kuhusu kuongeza idadi ya watalii wanaokuja, sisi kama Bunge tunampongeza Rais kwa hatua anazochukua kwenye hili eneo,” amesema Spika Tulia.

Aidha, Spika Tulia amewataka wabunge wafuatilie ziara ya Rais Samia nchini Marekani, ili waweze kujua namna ya kushauri kwa ajili ya uboreshaji wa suala hilo.

“Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii itakuja baadae, ni muhimu kila mbunge afuatilie mambo yanayoendelea huko ili kama kutakuwa na la kushauri hapa na pale, itakuwa rahisi zaidi. Baada ya kujua hatua mbalimbali zitakazochukuliwa na zile mnazotamani ziongezeke,” amesema Spika Tulia na kuongeza:

“Baada ya hapo ni muhimu kufuatilia ziara hii ya Rais Marekani ya kutangaza Taifa letu Tanzania.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!