Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Somalia yamtimua mjumbe wa Umoja wa Mataifa
Kimataifa

Somalia yamtimua mjumbe wa Umoja wa Mataifa

Nicholas Haysom
Spread the love

SERIKALI ya Somalia imemfukuza Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Mataifa (U.N) nchini humo, Nicholas Haysom kwa sababu ya kuingilia mambo ya ndani ya taifa hilo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Somalia, Haysom anadaiwa kuingilia wazi wazi masuala yake ya ndani.

Wizara hiyo imeeleza kuwa, imetoa taarifa za kufukuzwa kwa mwakilishi huyo kwa Katibu Mkuu wa U.N, Antonio Guterres.

Hivi karibuni vyombo vya habari nchini Somalia, viliripoti kwamba Haysom aliitaka serikali kutoa maelezo kuhusu kushikiliwa kwa wafuasi 15 na kiongozi wa zamani wa kundi la kigaidi la Al-Shabab ambaye aliwahi kushriki kinyang’anyiro cha uchaguzi wa nchi hiyo, Mukhtar Robow.

Haysom aliteuliwa na Guterres kuwa mwakilishi wa U.N nchini Somalia mnamo mwezi Septemba mwaka 2018.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!