Tuesday , 26 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Somalia yamtimua mjumbe wa Umoja wa Mataifa
Kimataifa

Somalia yamtimua mjumbe wa Umoja wa Mataifa

Nicholas Haysom
Spread the love

SERIKALI ya Somalia imemfukuza Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Mataifa (U.N) nchini humo, Nicholas Haysom kwa sababu ya kuingilia mambo ya ndani ya taifa hilo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Somalia, Haysom anadaiwa kuingilia wazi wazi masuala yake ya ndani.

Wizara hiyo imeeleza kuwa, imetoa taarifa za kufukuzwa kwa mwakilishi huyo kwa Katibu Mkuu wa U.N, Antonio Guterres.

Hivi karibuni vyombo vya habari nchini Somalia, viliripoti kwamba Haysom aliitaka serikali kutoa maelezo kuhusu kushikiliwa kwa wafuasi 15 na kiongozi wa zamani wa kundi la kigaidi la Al-Shabab ambaye aliwahi kushriki kinyang’anyiro cha uchaguzi wa nchi hiyo, Mukhtar Robow.

Haysom aliteuliwa na Guterres kuwa mwakilishi wa U.N nchini Somalia mnamo mwezi Septemba mwaka 2018.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Uvamizi wa kijeshi Milango ya bahari ya Taiwan G7 yapinga China

Spread the loveMKUTANO wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa nchi za...

Kimataifa

Rais Kagame kuwania muhula wa nne

Spread the loveRais wa Rwanda, Paul Kagame amesema atawania muhula wa nne...

Kimataifa

Ukraine kufungua kituo cha nafaka Kenya

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto amesema serikali ya Ukraine inapanga...

Kimataifa

Kufungwa kwa mpaka wa Tibet kulivyoathiri maisha ya Wanepali katika vijiji vya milimani

Spread the love  KALU Dhami kutoka Dhalain moja ya kata ya Manispaa...

error: Content is protected !!