SIRI ya Hamza Hassan Mohamed kumudu kutumia silaha na kuwaua askari watatu wa jeshi la polisi na mlinzi mmoja wa kampuni ya ulinzi ya SGA jijini Dar es Salaam kisha mwenyewe kuuawa, imebainika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Muuaji huyo ambaye uchunguzi wa tukio lake linaendelea kuchunguzwa na Jeshi la Polisi aliibua maswali mengi likiwamo wapi alikopata uwezo wa kutumia silaha za moto kwa namna alivyoonesha.
Lakini pia bado kuna maswali ambayo yanaendelea kuzunguka katika vichwa vya Watanzania ni kwanini aliamua kushambulia askari polisi pekee huku wananchi wengi wakiwepo.
Siku ya tukio hilo, Jumatano ya wiki iliyopita, Hamza alitumia bastola yake binafsi kuwafyatulia risasi askari polisi hao na kusababisha vifo vyao papo hapo.
Baada ya kuwaua, Hamza alipora silaha mbili bunduki aina ya AK 47 ambapo moja aliitundika shingoni, bastola kuunoni na bunduki nyingine aliishika mbele yake.
Undani wa habari hii soma Gazeti la Raia Mwema toleo la leo Jumatatu tarehe 30 Agosti 2021.
Headline not reflect your story (Wrong headline)
Tumpongeze shujaa wetu, tunastahiki kujenga mnara wa kumbukumbu ili tuzidi kumkumbuka kwa ushujaaa wake wa kuuwa mbwa poli zaid ya wa nne, hakika Hamza ni jasiri anaye stahiki kukumbukwa milele daima kwa jinsi alivyowenza kujitoa muhanga katika kupigania haki na uonevu, allah ailaze roho ya marehem mahala pemaaa pepon Aaameeen.
Siri ipi iliyofichuka hapo.
Achane kutengeneza vichwa ambavyo havina uhusiano na kilichomo.
Au mimi ndiyo sijaelewa vizuri. Nisaidieni rafiki zangu. Hii taarifa ina uhusiano na kichwa chake kwa namna gani?
Rafiki yako,
Aliko Musa
Mbobezi Kwenye Ardhi Na Majengo
HUYO mwandishi ni kanjanjala