Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Siri ya uwezo wa Hamza kutumia AK47 yafichuka
Habari MchanganyikoTangulizi

Siri ya uwezo wa Hamza kutumia AK47 yafichuka

Hamza Mohamed, aliyefyatulia risasi Polisi na kuwaua
Spread the love

 

SIRI ya Hamza Hassan Mohamed kumudu kutumia silaha na kuwaua askari watatu wa jeshi la polisi na mlinzi mmoja wa kampuni ya ulinzi ya SGA jijini Dar es Salaam kisha mwenyewe kuuawa, imebainika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Muuaji huyo ambaye uchunguzi wa tukio lake linaendelea kuchunguzwa na Jeshi la Polisi aliibua maswali mengi likiwamo wapi alikopata uwezo wa kutumia silaha za moto kwa namna alivyoonesha.

Lakini pia bado kuna maswali ambayo yanaendelea kuzunguka katika vichwa vya Watanzania ni kwanini aliamua kushambulia askari polisi pekee huku wananchi wengi wakiwepo.

Siku ya tukio hilo, Jumatano ya wiki iliyopita, Hamza alitumia bastola yake binafsi kuwafyatulia risasi askari polisi hao na kusababisha vifo vyao papo hapo.

Baada ya kuwaua, Hamza alipora silaha mbili bunduki aina ya AK 47 ambapo moja aliitundika shingoni, bastola kuunoni na bunduki nyingine aliishika mbele yake.

Undani wa habari hii soma Gazeti la Raia Mwema toleo la leo Jumatatu tarehe 30 Agosti 2021.

4 Comments

  • Tumpongeze shujaa wetu, tunastahiki kujenga mnara wa kumbukumbu ili tuzidi kumkumbuka kwa ushujaaa wake wa kuuwa mbwa poli zaid ya wa nne, hakika Hamza ni jasiri anaye stahiki kukumbukwa milele daima kwa jinsi alivyowenza kujitoa muhanga katika kupigania haki na uonevu, allah ailaze roho ya marehem mahala pemaaa pepon Aaameeen.

  • Siri ipi iliyofichuka hapo.

    Achane kutengeneza vichwa ambavyo havina uhusiano na kilichomo.

    Au mimi ndiyo sijaelewa vizuri. Nisaidieni rafiki zangu. Hii taarifa ina uhusiano na kichwa chake kwa namna gani?

    Rafiki yako,

    Aliko Musa

    Mbobezi Kwenye Ardhi Na Majengo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!