Friday , 2 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Sinema ya Kubenea kama ya Mbowe, Bulaya
Habari za SiasaTangulizi

Sinema ya Kubenea kama ya Mbowe, Bulaya

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo (Chadema)
Spread the love

SINEMA ya kukamatwa wabunge wa upinzani na kuwasafirisha kwa ndege wakiwa chini ya ulinzi mkali wa Polisi imejirudia leo  baada ya  Mbunge wa Ubungo,  Saed Kubenea (Chadema), kusafirishwa  alfajiri kwenda mjini   akitokea  jijini Dar es Salaam, anaandika Mwandishi wetu.

Kubenea amefikishwa mjini Dodoma baada ya jana kukamatwa akiwa hospitali  jijini Dar es Salaam alipoenda kupata matibabu na kulazwa kituo cha Polisi cha Oysterbay kabla ya leo alfajiri kupandishwa ndege kwenda kutoa maelezo mbele ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Bunge.

Mbunge huyo amekamatwa kwa amri ya Spika Job Ndugai ambaye wiki iliyopita aliviagiza vyombo vya dola kumsaka popote alipo Mbunge huyo na kumkamata.

Kosa la kukamatwa Kubenea lilitokana na kutofautina na Spika kuhusu idadi halisi ya risasi alizopigwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu mjini Dodoma .

Mbunge huyo alisema Lissu alipigwa risasi 38, huku Spika akisema idadi  ilikuwa 32 na baada ya kupishana huko, aliagiza Kubenea akamatwe ili akatoe ushahidi kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Bunge ambayo pia inaendelea kuchunguza tukio hilo.

Kukamtwa kwa Kubenea kunaonekana kama Sinema ambayo imezoelekwa kwa kuwa siyo mara ya kwanza wabunge wa upinzani kusafirishwa kwa ndege chini ya ulinzi mkali wa polisi.

Miongoni waliowahi kusafirishwa kwa ndege ni pamoja na Ester Bulaya  ambaye ni Mbunge wa Bunda (Chadema),  kwa amri ya Spika pamoja na Freeman Mbowe aliyesafirishwa kwa ndege pia kwenda jijini Arusha kuhudhuria kwenye kesi.

Taarifa zinasema Kubenea amewasili leo mjini Dodoma saa moja asubuhi na kwamba badio afya yake siyo nzuri na hivyo hajui kama anaweza kusimama na kuhojiwa na kamati hiyo.

Aidha, taarifa hiyo imesema Kubenea bado ana maumivu makali sana na kwamba hajaambiwa atahojiwa wapi na saa ngapi.

Kubenea amemshukuru Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na  Mandeleo ya Makazi, Angelina Mabula ambaye amesema amesaidia katika hali yake ya ugonjwa mpaka kufika Dodoma baada ya kukutana naye kwenye ndege leo asubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

error: Content is protected !!