NI mikasa na maajabu inayoandika historia, katika kijiji cha Kiponzelo mkoani Iringa nchini Tanzania. Anaripoti Hamisi Mguta, Iringa … (endelea).
Kijiji ambacho kina mapango ya ajabu ambayo watu wamekuwa wakisikika kucheza ngoma ndani yake lakini hawakuwahi kuonekana.
Wapo waliotoa ushuhuda wa kupotea juu ya jiwe kubwa, baada ya kwenda kushuhudia kisima kilichopatikana juu ya jiwe hilo ambacho hakijawahi kukauka miaka nenda rudi.
Na inasemekana pia kuna nyoka mkubwa mwenye vichwa 12 ambaye hupiga kelele za ajabu ifikapo mwezi wa Julai kila mwaka.
Ni takriban umbali wa kilomita 54, kutoka Iringa mjini hadi kufika katika Kijiji hiki chenye historia lukuki zitakazokuacha mdomo wazi.
Undani wa simulizi hii, tazama video hii, mwanzo hadi mwisho.
Leave a comment