RAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amemuapisha Jenista Mhagama kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 2 Aprili, 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Pia amemuapisha George Simbachawene kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Jana tarehe 1 Aprili 2023 Rais Samia alifanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri kwa kumteua Jenista Mhagama kuwa Waziri wa Wizara hiyo na George Simbachawene kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, ambapo kabla ya uteuzi huo Simbachawene alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu).
Leave a comment