Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Simbachawene awaitia fulsa watu Dodoma
Habari Mchanganyiko

Simbachawene awaitia fulsa watu Dodoma

Jengo la Bunge la Tanzania mjini Dodoma
Spread the love

WAZIRI  wa Nchi Ofisi ya Rais  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene amewataka wananchi kuchangamkia fursa za kimaendeleo zinazopatikana katika mkoa wa Dodoma kutokana na uwepo kwa makao makuu, anaandika Dany Tibason.

Mbali na kuwataka kuchangamkia fursa kiongozi huyo, amewataka wananchi kuacha tabia ya kubweteka na kusubiria misaada kutoka kwa wafadhili.

Alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati wa uzinduzi wa Benki ya  DCB Commercial Bank uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa LAPF mjini Dodoma.

Simbachawene amesema ili kuondokana na umasikini ni vyema kila mtanzania kuhakikisha anafanya kazi huku wakichangamkia fursa ambazo zinatokana na taasisi za kibenki.

Kutokana na Dodoma kuwa makao maku ya nchi kuna kila sababu ya kutumia taasisi za kifedha kwa ajili ya kuomba mikopo kwa lengo la kujiendeleza kiuchumi.

“Lazima Dodoma ipewe kipaumbele ya kujiendeleza kiuchumi na mfano mzuri sasa ni kuitumia benki ya DCB  abayo kwa sasa imezinduliwa rasm katika mkoa wa Dodoma kutoka na umuhimu Dodoma kuwa makao makuu.

Akizungumzia DCB aliwataka wananchi kujiunga na benki hiyo ili kuweza kufungua akaunti ili kuweza kupata mkopo kwa masharti nafuu pamoja na kutoza riba kidogo ambayo ni miatano kwa mwezi.

Kwa upande wake mkurugenzi wa Benki ya DCB,Edson Mkwawa amesema bnki hiyo inalenga kuwakomboa wananchi ili kuhakikisha wanapata mikopo ya riba nafuu kwa lengo la kujikwamua kiuchumi.

Amesema ili wananchi waweze kuondokana na umasikini ni jambo jema wakajiunga katika vikundi pamja na kukopa mikopo kwa riba nafuu zaidi kwa lengo la kujiongezea kipata.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!