Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Michezo Simba yawasili kibabe DR Congo, kuikabili AS Vita
Michezo

Simba yawasili kibabe DR Congo, kuikabili AS Vita

Spread the love

 

MSAFARA wa wachezaji, benchi la ufundi pamoja na viongozi wa klabu ya Simba umewasili salama Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo leo tarehe 10 Februari 2021, kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya AS Vita Club. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa kwanza wa kundi A, utachezwa siku ya Ijumaa tarehe 12 Februari majira ya saa 1 usiku kwenye Uwanja wa Stade des Martyrs.

Simba iliondoka jana nchini kupitia Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere majira ya saa 10 jioni ikiwa na msafara wa watu 44, kuelekea Ethiopia na leo asubuhi majira ya saa 10 asubuhi iliunganisha ndege na kuelekea Kinshasa, DR Congo.

Ikumbukwe mara ya mwisho kwa Simba kukutana na AS Vita Club kwenye uwanja huo ilikuwa msimu wa 2018/19 na kupoteza mchezo huo kwa mabao 5-0, licha ya kufanikiwa kufuzu kwenye hatua ya robo fainali.

Wachezaji pekee walioachwa kwenye msafara huo ni nahodha wao John Bocco ambaye anasumbuliwa na majeruhi pamoja na kiungo mshambuliaji wao Perfect Chikwende ambaye kanuni za mashindano hayo hazimruhusu kucheza mara baada ya uhamisho wake kutoka FC Platinum ya Zimbabwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!