Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari Simba yawasili Afrika kusini, walia kunyimwa Askari
HabariMichezo

Simba yawasili Afrika kusini, walia kunyimwa Askari

Spread the love

 

KLABU ya Simba imewasili salama nchini Afrika Kusini kwenye mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Orlando Pirates, huku wakilalamika kuwa wenyeji hao wameshindwa kuwapatia polisi wa kuwaongoza barabarani (Escort). Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo wa wa marudiano wa robo fainali utapigwa siku ya Jumapili, Aprili 24, 2022 kwenye dimba la Orlando lililopo Soweto, jijini Johannesburg.

Simba ambao waliondoka nchini leo asubuhi, kupitia kurasa za mitandao ya kijamii walitoa taarifa hiyo ya kuwasili Afrika Kusini, na kuwashukuru wenyeji wao hao kwa mapokezi licha ya kutowapatia Askari.

“Asanteni Orlando Pirates kwa mapokezi lakini mmetunyima polisi wa kutuongoza barabarani (Escort) hivyo tumelazimika kutumia gari la Balozi wa Tanzania nchini Afrika ya kusini kutuongoza”

Simba wanaingia kwenye mchezo huo siku ya Jumapili, huku wakiwa na kumbukumbu ya kupata ushindi kwenye mchezo wa kwanza kwa bao 1-0, uliopigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Kwenye mchezo huo Simba inahitaji sare ya aina yoyote, ili kuweza kufuzu kwa hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

error: Content is protected !!