Maraba baada ya mapumziko siku tano kikosi cha mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara kimeanza tena mazoezi kwa ajili ya ungwe ya mwisho ya michezo ya ligi Kuu Tanzania Bara ambayo inaelekea mwishoni. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Simba iliingia kambini jana huku baadhi ya wachezaji wakiwa kwenye majukumu ya timu zao Taifa ambazo zinataraijia kucheza michezo ya kirafiki hivi karibuni kwa mujibu wa kalenda ya Shiriukisho la mpira wa Miguu Duniani (FIFA)
Wachezaji hao walipewa mapumziko mara baada ya kucheza mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Ruvu Shooting uliopigwa kwenye Uwanja wa Ccm Kirumba, Mwanza na Simba kuibuka na ushindi wa mabao 3-0.
Katika mazoezi hayo kikosi cha Simba kitakuwa chini ya kocha wao wa viungo Adel Zrane na kisha baadae kucheza michezo kadhaa ya kirafiki ambayo haikuwekwa wazi kabla ya kurejea kwenye mchezo wa Ligi Kuu tarehe 19 Juni 2021, dhidi ya Polisi Tanzania.
Simba mpaka sasa ndio vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara wakiwa na pointi 67, mara baada ya kucheza michezo 27 na nafasi ya pili wakiwa watani zao Yanga wakiwa na pointi 61 na michezo 29.
Simba imebakiza michezo mitano kwenye ligi hiyo ambao ni dhidi ya Polisi Tanzania, Azam Fc, Yanga, Mbeya City na Kmc.
Leave a comment