BODI ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania imefanya mabadiliko ya ratiba ya Ligi Kuu Bara ikiwa ni wiki mbili kabla ya kuanza kwa ligi hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura amesema wamelazimika kupangua ligi hiyo kutokana na baadhi ya viwanja vilivyopangwa kufanyika kwa michezo ya ligi hiyo kuwa na shughuli za kijamii.
Mchezo wa ufunguzi kati ya Simba na Tanzania Prison uliopangwa kufanyika 22 Agosti, 2018 katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Saalam, umehamishiwa kwenye Uwanja wa Uhuru tarehe hiyo hiyo kutokana na kuwepo na shughuli za kijamii ndani ya uwanja uliopangwa awali.
Aidha mchezo mwengine wa mzunguko wa kwanza wa ligi uliokuwa uwakutanishe Mtibwa Sugar na Yanga katika dimba la Jamhuri Morogoro 23 Agosti, utachezwa kwenye uwanja wa Uhuru na Yanga atakuwa mwenyeji kwenye mchezo huo kutokana na uwanja wa Jamhuri kuwa na shughuli za kijamii mpaka 30 Agosti mwaka huu.
Mabadiliko haya yamekuja kufuatia asilimia 90 za klabu zinazoshiriki ligi kuu Tanzania bara hazimiliki viwanja vyao binafsi bali hutumia viwanja vinavyo milikiwa na serikalai pamoja na Chama Cha Mapinduzi.
Leave a comment