Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Simba, Yanga kufanya mazoezi uwanja mmoja Kigoma
Michezo

Simba, Yanga kufanya mazoezi uwanja mmoja Kigoma

Wachezaji wa Yanga wakiwa mazoezini
Spread the love

 

KUELEKEA mchezo wa fainali wa Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation) siku ya tarehe 25 Julai, 2021, vikosi vya Simba na Yanga vitatumia uwanja mmoja wa mazoezi kwa nyakati tofauti. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Kigoma … (endelea).

Mchezo huo utapigwa kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika majira ya saa 10 jioni.

Uamuzi huo, umefikiwa mara baada ya kufanyika kwa kikao cha kamati ya mashindano siku ya Jumatatu na kukubaliana timu hizo zitumie Uwanja wa chuo cha Hali ya Hewa, Kigoma.

Yanga ndiyo watakaokuwa wa kwanza kutumia uwanja huo kwenye mazoezi yake ya kwanza toka walipowasili Kigoma, majira ya saa 1 asubuhi kwa usafiri wa Shirika la Ndege la Tanzania.

Kikosi cha Simba kikifanya mazoezi

Simba wao wataanza mazoezi siku ya kesho, baada kutua mkoani Kigoma jioni ya leo wakitokea Dar es Salaam.

Kutumia uwanja huo mmoja kumekuja kufuatia kwa klabu hizo kutoruhusiwa kufanya mazoezi kwenye uwanja wa Lake Tanganyika ambao utachezewa mchezo huo.

Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ndani ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Salum Madadi alisema kuwa hawatoruhusu timu yoyote kutumia uwanja huo mpaka siku ya mchezo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!