Wednesday , 17 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba, Yanga kufanya mazoezi uwanja mmoja Kigoma
Michezo

Simba, Yanga kufanya mazoezi uwanja mmoja Kigoma

Wachezaji wa Yanga wakiwa mazoezini
Spread the love

 

KUELEKEA mchezo wa fainali wa Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation) siku ya tarehe 25 Julai, 2021, vikosi vya Simba na Yanga vitatumia uwanja mmoja wa mazoezi kwa nyakati tofauti. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Kigoma … (endelea).

Mchezo huo utapigwa kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika majira ya saa 10 jioni.

Uamuzi huo, umefikiwa mara baada ya kufanyika kwa kikao cha kamati ya mashindano siku ya Jumatatu na kukubaliana timu hizo zitumie Uwanja wa chuo cha Hali ya Hewa, Kigoma.

Yanga ndiyo watakaokuwa wa kwanza kutumia uwanja huo kwenye mazoezi yake ya kwanza toka walipowasili Kigoma, majira ya saa 1 asubuhi kwa usafiri wa Shirika la Ndege la Tanzania.

Kikosi cha Simba kikifanya mazoezi

Simba wao wataanza mazoezi siku ya kesho, baada kutua mkoani Kigoma jioni ya leo wakitokea Dar es Salaam.

Kutumia uwanja huo mmoja kumekuja kufuatia kwa klabu hizo kutoruhusiwa kufanya mazoezi kwenye uwanja wa Lake Tanganyika ambao utachezewa mchezo huo.

Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ndani ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Salum Madadi alisema kuwa hawatoruhusu timu yoyote kutumia uwanja huo mpaka siku ya mchezo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!