Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba, Yanga hakuna mbabe
Michezo

Simba, Yanga hakuna mbabe

Spread the love

 

MTANANGE wa watani wa jadi kati ya Simba na Yanga uliopigwa leo tarehe 11 Disemba 2021, katika dimba la Mkapa jijini Dar es Salaam, umemalizika kwa sare tasa (0-0). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam  …  (endelea).

Katika mechi hiyo iliyokuwa ya kuvutia, kila timu ilionesha mbinu za hali ya juu kuzuia mashambulizi ya mwenziwe na kuwafanya mashabiki wao kuamini kila moja anaweza kuondoka na ushindi.

Licha ya kipindi cha kwanza Yanga kuonekana kuwa imara haikuambulia kitu licha ya mashuti yake mawili kulenga lango la Simba.

Vivyo hivyo, Simba walionekana kuimarika zaidi kipindi cha pili na kufanya mashambulizi ambapo mashuti matatu yalilenga lango lakini hawakuwa na bahati.

Hadi dakika 90 zinakatika wachezaji watatu wa Simba walikuwa wamelamba kadi za njano huku wawili wa Yanga nao pia wakipewa kadi hizo za onyo.

Umiliki wa mpira unaonesha Yanga wameongeza kwa kuwa na asilimia 51 dhidi ya 49 za Simba.

Hata hivyo, manahodha wa pande zote mbili, Medie Kagere wa Simba na Bakari Mwamnyeto wa Yanga wamekiri kuwa mechi ilikuwa ngumu lakini kwani ilikuwa ni mechi ambayo ilikuwa kiufundi zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!