Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Simba yamshusha mrithi wa Miquissone
Michezo

Simba yamshusha mrithi wa Miquissone

Spread the love

 

KLABU ya Simba, imefanikiwa kunyakuwa winga wa kimataifa wa Malawi, Duncan Nyoni ambaye amejiunga rasmi na kikosi hiko, kwa ajili ya msimu mpya wa mashindano. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezaji huyo ambaye anacheza nafasi ya winga, pamoja na mshambuliaji ametambulishwa hii leo na huenda akaja kuchukua nafasi ya Luis Miquissone aliyetimkia Al Ahly.

Simba inafanya usajili huo, huku kikosi chao kikiwa jijini Rabat nchini Morocco kwenye maandalizi kwa ajili ya msimu ujao wa mashindano.

Duncan mwenye umri wa miaka 23, amejiunga na Simba akitokea kwenye klabu ya Silver Strikers ya nchini Malawi kama mchezaji huru.

Simba inafanya usajili huo huku tayari ikiwa imeondokewa na wachezaji wake wawili ambao ni Miquisone pamoja na kiungo wake, Clatous Chama aliyetimkia kwenye klabu ya RS Berkane.

Miquissone amejiunga Al Ahly kwa ada ya uhamisho ya shilingi 2.3 bilioni, ambayo klabu ya Al Ahly imetoa kwenda Simba.

Kwa upande wa Chama tayari ameshajiunga na na club ya RS Berkane ya nchini Morocco kwa mkataba wa miaka mitatu.

Chama amesaini mkataba huo unaotajwa kuwa umeigharimu RS Berkane ada ya uhamisho ya Tsh Bilioni 1.5 kwenda Simba SC na kuongezewa mshahara mara nne ya aliokuwa analipwa Simba SC.

Chama ambae ameonekana kwenye mazoezi ya RS Berkane akiwa na Tuisila Kisinda wa Yanga, alijiunga na Simba SC mwaka 2018 akitokea Lusaka Dynamos ya Zambia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!