Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba yaipiga Kaizer Chiefs 3, yaaga mashindano
MichezoTangulizi

Simba yaipiga Kaizer Chiefs 3, yaaga mashindano

Spread the love

PAMOJA na ushindi wa bao 3-0 walioupata kkabu ya Simba dhidi ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini, lakini mabingwa hao wa Ligi Kuu Tanzania Bara wameaga mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa jumla ya mabao 4-3. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Simba ambao walipoteza mchezo wa kwanza wa robo fainali uliochezwa Afrika Kusini wiki iliyopita kwa mabao 4-0, walikuwa wanahitaji ushindi wa mabao 5-0.

Kampeni ya Simba kusaka tiketi ya nusu fainali katika Uwanja wa Benjamin Mkapa ilianza dakika ya 23 kwa John Bocco kuandika bao la kwanza na kufanya mchezo kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa bao 1-0.

Simba walirudi kwa kasi kipindi cha pili na kufanikiwa kupata bao la pili dakika ya 56 akiunganisha krosi fupi ya Mohammed Hussein.

Wakati Kaizer Chiefs wakicheza mchezo wa kuzhia zaidi huku wakipoteza muda, Simba waliendelea kulisakama lango la wapinzani wao na kufanikiwa kupata bao la tatu kupitia kwa Claytous Chama dakika ya 85.

Hadi kipenga cha mwisho matokeo yalibaki kuwa Simba mabao matatu ambayo yameshindwa kuwasaidia kusonga mbele katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!