Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba yaifunga Kagera 2-1, yatinga robo fainali
Michezo

Simba yaifunga Kagera 2-1, yatinga robo fainali

Spread the love

 

MABIGWA watetezi wa Kombe la Shirikisho Azam Federation CUP (ASFC), Simba ya Dar es Salaam, imetinga robo fainali ya michuano hiyo, baada ya kuibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Kagera sugar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Simba imeibuka na ushindi huo leo Jumamosi, tarehe 1 Mei 2021, katika mchezo huo, uliochezwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, mkoani Dar es Salaam.

Kagera ilikuwa ya kwanza kujipatia goli, dakika ya 45, kupitia kwa Erick Mwijage akiunganisha pasi kwa kichwa ya Dickson Muhilu.

Timu hizo, zilikwenda mapumziko kwa Kagera ikiongoza 1-0.

Dakika 45 za kipindi cha pili, zilianza kwa kushuhudia, Kocha wa Simba, Didier Gomez, akimtoa kiungo mkabaji, Thadeo Lwanga na kumwingiza, Bernard Morrison, ambapo aliifanya Simba kuanza kulishambulia kwa kasi lango la Kagera.

Simba iliwachukua dakika kumi tangu kuanza kwa kipindi cha pili, ambapo Morrison aliisawazishia timu yake dakika ya 55 kwa kuunganisha pasi ya Louis Miquissone.

Dakika ya 67, Meddie Kagera aliifungia Simba goli la pili na la ushindi, akiunganisha pasi safi ya Morrison.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!