Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Simba yaifunga Kagera 2-1, yatinga robo fainali
Michezo

Simba yaifunga Kagera 2-1, yatinga robo fainali

Spread the love

 

MABIGWA watetezi wa Kombe la Shirikisho Azam Federation CUP (ASFC), Simba ya Dar es Salaam, imetinga robo fainali ya michuano hiyo, baada ya kuibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Kagera sugar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Simba imeibuka na ushindi huo leo Jumamosi, tarehe 1 Mei 2021, katika mchezo huo, uliochezwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, mkoani Dar es Salaam.

Kagera ilikuwa ya kwanza kujipatia goli, dakika ya 45, kupitia kwa Erick Mwijage akiunganisha pasi kwa kichwa ya Dickson Muhilu.

Timu hizo, zilikwenda mapumziko kwa Kagera ikiongoza 1-0.

Dakika 45 za kipindi cha pili, zilianza kwa kushuhudia, Kocha wa Simba, Didier Gomez, akimtoa kiungo mkabaji, Thadeo Lwanga na kumwingiza, Bernard Morrison, ambapo aliifanya Simba kuanza kulishambulia kwa kasi lango la Kagera.

Simba iliwachukua dakika kumi tangu kuanza kwa kipindi cha pili, ambapo Morrison aliisawazishia timu yake dakika ya 55 kwa kuunganisha pasi ya Louis Miquissone.

Dakika ya 67, Meddie Kagera aliifungia Simba goli la pili na la ushindi, akiunganisha pasi safi ya Morrison.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!