Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Simba yafufua matumaini Klabu Bingwa
Michezo

Simba yafufua matumaini Klabu Bingwa

Spread the love

BAO la Meddy Kagere katika dakika ya 64 ya mchezo wa Klabu Bingwa Afrika kati ya Simba dhidi ya Al Ahly kutoka Misri lilitosha kufufua matumaini ya kusonga mbele kwenye hatua ya robo fainali. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea)

Simba ambayo ilionekana kupoteza matumaini hapo awali baada ya kupoteza katika michezo miwili ya ugenini dhidi ya AS Vital na Al Ahly ilijitahidi kupambana katika dakika zote 90 za mchezo kwa kumiliki mpira asilimia kubwa na hatimaye wakaibuka na ushindi.

Baada ya mchezo kumaliza kocha wa klabu ya Simba Patrick Aussems alisema alitumia muda mwingi kuwaonesha wachezaji wake video ya mchezo waliopoteza Misri kwa mabao 5-0 na kuona namna gani wanaweza kurekebisha makosa.

“Niliwaonesha baadhi ya video ni kivipi Al Ahly wanacheza na tukaweza kujipanga vizuri na tulikuwa na mipango mizuri na tumebakisha mechi mbili na tutaona matokeo yake,” alisema kocha huyo.

Baada ya ushindi huo sasa Simba inafikisha jumla ya pointi sita baada ya kushinda michezo miwili na kushika nafasi ya pili kwenye msimamo wa kundi D.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!