Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Simba yabadilishiwa muda wa mechi Sudan, sasa kukipiga saa 9
MichezoTangulizi

Simba yabadilishiwa muda wa mechi Sudan, sasa kukipiga saa 9

Spread the love

KIKOSI cha wachezaji 25 wa Simba pamoja na viongozi kimewasilini jijini Khartom nchini Sudan kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Al Merreikh huku muda wa kuchezwa mchezo huo ukibadilika kutoka saa 3 usiku na sasa utachezwa majira ya saa 10 kwa saa za Afrika mashariki na saa 9 kamili kwa saa za sudani. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mabadiliko ya muda huo yamethibitishwa na mtendaji mkuu wa klabu hiyo Barbara Gonzalenz kupitia ukurasa wake wa Instagram na kuandika kuwa “Tupo njiani kuelekea Khartoum, Sudan kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya mabingwa dhidi ya Al Merreikh, muda wa mechi umebadilika”

Simba imewasili leo alfajili nchini Sudan na kuanza maandalizi ya mchezo huo wa kundi A, ambapo mpaka sasa wao ndio vinara kwenye kundi hilo wakiwa na pointi sita mara baada ya kuibuka na ushindi katika michezo yao miwili ya awali, dhidi ya As Vita na Al Ahly.

Al Merreikh wanaingia kwenye mchezo huo huku wakiwa na kumbukumbu ya kupoteza katika mechi mbili za awali mara baada ya kukubali kichapo cha mabao 3-0 dhidi ya Al Ahly kwenye mchezo wa kwanza na baadae kufungwa mabao 4-1 kwenye mchezo wa nyumbani dhidi ya AS Vita kutoka Congo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!