MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara, klabu ya soka ya Simba imeachana rasmi na kocha wake Pablo Franco Martni mara baada ya kufikia makubaliano ya pande zote mbili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)
Makubaliano hayo yamefikiwa hii leo tarehe 31 Mei 2022, huku klabu hiyo ikimtakia kila la kheri katika maisha yake mapya nje ya klabu hiyo.
Pablo alijiunga na Simba tarehe 10 Novemba 2022, Akichukua nafasi ya Didier Gomes, ambaye aliamua kuachana na timu hiyo kufutai matokeo mabaya aliyoyapata kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika kwenye msimu huu.
Aidha uongozi wa timu hiyo pia imevunja mkataba na kocha wake wa viungo Daniel De Castro Reyes Ambaye alijiunga na timu hiyo sambamba na Pablo.
Taarifa iliyotolewa na uongozi wa timu hiyo imeeleza kuwa, kwa sasa kikosi cha Simva kitakuwa chini ya mwalimu wao msaidizi Selamani Matola kwenye michezo mitano ya Ligi iliyosalia.
Pablo amevunjiwa mkataba wake siku chache, mara baada ya kupoteza pambano la nusu fainali ya kombe la Shirikisho dhidi ya Yanga lililofanyika jijini Mwanza, mara baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0.
Toka alipofika nchini Pablo amefanikiwa kuwapa Simba taji moja tu, la michuano ya kombe la Mapinduzi mara baada ya kuwafunga Azam FC kwenye fainali.
Leave a comment