Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Simba uso kwa uso na Al Ahly, AS Vita na El Merreikh
Michezo

Simba uso kwa uso na Al Ahly, AS Vita na El Merreikh

Kikosi cha Simba
Spread the love

KLABU ya Soka ya Simba imepangwa kundi A, kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika pamoja na klabu za Al Ahly kutoka nchini Misri, AS Vita kutoka DR Congo na Al Merreikh ya nchini Sudan. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Makundi hayo yamepangwa leo tarehe 8 Januari, 2021 kwenye droo iliyochezeshwa jijini Cairo, Misri ambapo Simba imepangwa tena na bingwa mtetezi wa michuano hii klabu ya Al Ahly pamoja na AS Vita ambao Simba alicheza nao mara ya mwisho aliposhiriki hatua hii ya raundi kwenye msimu wa 2018/19 na Simba alifanikiwa kufuzu hatua ya nane bora.

Kikosi cha Al Ahly

Kwenye kundi hilo Simba ataanza mchezo wa kwanza ugenini dhidi ya AS Vita kutoka Congo ambapo mara ya mwisho kucheza dhidi ya timu hiyo Simba alifungwa mabao 5-0, na mara baada ya hapo Simba atarejea nyumbani Tanzania kuwakabili Al Ahly kutoka nchini Misri ambapo mara ya mwisho Simba alipata ushindi wa bao1-0.

Kikosi cha AS Vita

Mara ya mwisho Simba kushiriki hatua ya makundi ilikuwa msimu wa 2018/19 alikuwa kundi D, dhidi ya timu za Al Ahly, AS Vita na JS Soura na Simba ikafanikiwa kumaliza kwenye nafasi ya pili na kwenda hatua ya rob0 fainali na kupoteza mchezo huo mbele ya TP Mazembe.

Al Merreikh ya Sudan

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!