Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Simba kushiriki michuano mipya Barani Afrika
Michezo

Simba kushiriki michuano mipya Barani Afrika

Spread the love

 

KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) itakutana Julai 16, 2021, nchini Morocco kujadili mfumo wa mashindano mapya ya (CAF Super League), ambayo Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Dunia (FIFA), Gianni Infantino ameyapa baraka. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Michuano hiyo inatarajia kushirikisha timu 20, ambapo kati ya hizo, timu 15 zimetajwa kushiriki ikiwemo Simba kutoka Tanzania.

Mashindano hayo, ambapo mapema mwaka huu yalishindikana kufanyika barani Ulaya (Europian Super League), sasa yamegeukia barani Afrika huku Rais wa sasa wa Shirikisho hilo, Patrice Motsepe akijinasibu kuwa yatakuza mpira wa Afrika.

Kwa mujibu wa mtandao wa Goal.com ulimnukuu Motsepe ambaye alinena kuwa dhumuni la michuano hiyo mipya limeshajadiliwa na wamejifunza kupitia barani Ulaya ambapo michuano hiyo ilishindikana.

“Tumeshafanya tathimini na mijadala ya awali itaanza na kuungwa mkono kwa mapana na wanufanika wa michuano hiyo.

Patrice Motsepe, Rais wa CAF

“Tumeangalia kwa namna gani, klabu kubwa barani Ulaya zilivyoshindwa kuunda michuano hiyo (European Super League) kutokana na uzoefu pamoja na changamoto zote walizopitia,” alifunguka Motsepe ambaye ameingia madarakani mwezi Machi, kuchukua nafasi ya Ahmad Ahmad.

Aidha Motsepe alisema kuwa anaamini wazo hilo, litasaidia kukuza mpira wa bara la Afrika ulimwenguni. “Itachangia mpira wa Afrika kuwa wa ushindani ulimwenguni,” alisema Rais huyo.

Michuano hiyo ambayo itakuwa na klabu 20 wanachama, na wengine wanaweza kushiriki kupitia michezo ya mtoano katika hatua ya awali.

Giann Infantino, Rais wa FIFA

Mtandao huo pia uliripoti kuwa Rais wa FIFA, Gian Infantino ambaye alipendekeza michuano hiyo kufanyika barani Afrika na kutabili kuwa baada ya miaka mitano wataingiza kiasi cha Sh. 6.9 trillioni.

Ukiacha Simba zingine timu ambazo mpaka sasa zitashiriki michuano hiyo ni Wydady na Raja Casablanca kutoka Morocco, Burkane, Al Ahly, Zamalek na Pyramids za Misri, Mamelod Sundowns, Orlando Pirates na Kaizer Chiefs kutoka Afrika Kusini.

Wengine ni TP Mazembe na AS Vita za nchini DR Congo, Al Hilal, Al Merreikh kutoka Sudan na Horoya ya nchini Guinea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!