KIKOSI cha klabu ya Simba leo kitashuka dimbani, kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya KMC, ambapo Kocha Msaidizi, Selaman Matola amesema wanataka kushinda mchezo huo ili kuwa mabingwa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Mchezo huo utapigwa kesho kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, majira ya saa usiku.
Akizungumza kuelekea mchezo huo, Matola alisema kuwa, mara baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Yanga, sasa wanaingia kwenye mechi dhidi ya Kmc na kukili kuwa utakuwa mchezo mgumu.
“Mara baada ya kucheza mchezo wetu dhidi ya Yanga na kupoteza, najua sasa tunaingia kwenye mechi ya KMC najua nayo ni ngumu sio rahisi.
“KMC ni timu ngumu, inawachezaji wazoefu wanaojielewa ila tujiandaa kupata matokeo pamoja na ugumu huo ili tuweze kuwa mabingwa,” amesema Matola.
Simba mpaka sasa inapointi 73, ikiwa kileleni mara baada ya kucheza michezo 30, ambapo wanahitaji pointi nne, ilikufikisha alama 77 ambapo hazitafikiwa na timu yoyote kwenye msimamo wa Ligi.
Aidha Matola alinena kuwa, kupoteza mchezo wao dhidi ya Yanga hawakupenda, ila imetokea kwa kuwa nao walikuwa wakihitaji pointi hizo kuwa mabingwa.
“Tumefungwa sio kama tumependa ila tunahitaji kupata matokeo ili tuwe mabingwa kwenye mechi ya kesho,” aliongezea Matola.
Leave a comment