Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Simba kukutana na timu hizi Robo Fainali
Michezo

Simba kukutana na timu hizi Robo Fainali

Spread the love

 

BAADA ya kukubali kichapo cha bao 1-0, dhidi ya Al Ahly na kumaliza nafasi ya kwanza kwenye kundi A, klabu ya Simba itacheza hatua ya robo fainali dhidi ya Cr Belouizdad, Horoya na MC Alger. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea). 

Simba atakutana na timu hizo ambazo zimeshika nafasi ya pili kwenye makundi yao na mchezo huo wa robo fainali wataanzia ugenini kwa sababu ni kinara wa kundi A.

Kwenye kundi A, Simba amemaliza akiwa na pointi 13 na nafasi ya pili ikishikwa na Al Ahly ikiwa na pointi 11.

Kwa mantiki hiyo kwenye mchezo wa robo fainali Simba atakuwa na faida ya kuanzia ugenini kati ya timu hizo tatu zilizoshika nafasi ya pili.

CR Belouizdad imeshika nafasi ya pili kwenye kundi B, nyuma ya Mamelodi Sundown wakiwa na pointi tisa, Holoya wao wameshika nafasi hiyo ya pili wakiwa kundi C, wakiwa na pointi 8, nyuma ya Wydad Casablanca.

MC Alger wameshika nafasi hiyo ya pili kwenye kundi D, wakiwa na pointi 8, nyuma ya ES Tunis iliyoongoza kundi hilo.

Michezo hiyo ya robo fainali itachezwa kuanzia tarehe 14 Mei 2021 na fainali ya michuano hiyo kwa msimu wa 2020/21 itachezwa tarehe 17 Julai, 2021.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!