Tuesday , 26 September 2023
Home Kitengo Michezo Simba kukipiga na Asante kotoko kutoka Ghana
Michezo

Simba kukipiga na Asante kotoko kutoka Ghana

Spread the love

MABINGWA wa Ligi Kuu Tanzani Bara, Simba wanatarajia kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Asante Kotoko kutoka Ghana katika maadhimisho ya siku ya Simba (Simba Day) yanayotarajia kufanyika katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam 8 Agosti 2018.

Akiongea na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa Hotel ya Serena, Mkuu wa idara ya Habari ndani ya klabu hiyo Haji Manara amesema kuwa hapo awali kulikuwa na taarifa ya kuwa watacheza na AFC Leopard kutoka Kenya lakini taarifa hiyo sio sahihi bali watakipiga na mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Ghana.

“Taarifa ambazo zilikuwa zikienea kwamba tutacheza dhidi ya AFC Leopard kutoka Kenya si za kweli na tutacheza na hiyo ambayo tumeitaja,” amesema Manara.

Licha ya hayo Msemaji huyo aliongezea ya kuwa katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya Simba day ndani ya wiki hii wanatarajia kufanya shughuli mbali mbali za kijamii.

Simba ambayo kwa sasa imeweka kambi nchini Uturuki kwa ajiri ya kujiandaa na msimu mpya kwa michuano ya ligi kuu na kombe la klabu bingwa barani Afrika ambao watakuwa wanawakilisha nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Piga pesa kupitia Derby ya London Kaskazini kwa kubadhiri na Meridianbet

Spread the love NAJUA umesikia na unazijua Derby nyingi kutoka jiji la London,...

BiasharaMichezo

Wikiendi hii ushindi upo Meridianbet na si kwingine

Spread the love USHINDI huu ni wako mteja wa Meridianbet kama mechi...

BiasharaMichezo

Safari ya Gavi kutoka Academy ya Real Betis mpaka Barca

Spread the love  ANITWA Pablo Martín Páez Gavira ‘Gavi’, sasa ni mchezaji...

BiasharaMichezo

SBL yazindua Serengeti Oktoba Festival

Spread the love  KAMPUNI ya Bia ya Serengeti Breweries Ltd (SBL) kupitia...

error: Content is protected !!