DROO ya 32 ya michuano ya kombe la Shirikisho la Azam imechezeshwa hii leo, ambapo bingwa mtetezi wa michuano hiyo klabu ya Simba itamenyana na Dar City, wakati huo Yanga watakuwa kibarua dhidi ya Mbao FC. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Michezo ya hatua hiyo inatarajiwa kupigwa kati ya tarehe 28-30 Januari, mwaka huu ambapo timu zitakazofuzu zitaingia moja kwa moja kwenye hatua ya 16 bora.
Katika hatua hiyo timu zinazoshiriki Ligi Kuu bara zipo 15, huku katika michezo miwili zitakutana wenyewe kwa wenyewe.
Mchezao wa kwanza utakaozikutanisha timu za Ligi utakuwa kati ya Biashara United ya Mara, dhidi ya Mbeya Kwanza na mchezo mwengine utakuwa Kmc ambao watawakabili Ruvu Shooting.
Ifutayo ni ratiba kamili ya michuano hiyo.
Leave a comment