Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Simba kuifuata Al Ahly jioni ya leo
Michezo

Simba kuifuata Al Ahly jioni ya leo

Spread the love

 

KIKOSI cha wachezaji pamoja na viongozi wa klabu ya Simba wataondoka jioni ya leo tarehe 6 Aprili, 2021, kuelekea nchini Misri kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa kundi A, utachezwa tarehe 9 Aprili, 2021 huku Simba ikiwa tayari imeshakata tiketi ya robo fainali ya michuano hiyo.

Kikosi hiki kitaondoka Jijini Dar es Salaam 9:25 na Shirika la ndege la Emirates mpaka Dubai na kisha kesho Jumatano asubuhi wataanza safari ya kwenda Cairo ambapo watafika majira ya 4:05 asubuhi.

Simba inaenda kucheza mchezo huo huku wakiwa vinara kwenye kundi A, wakiwa na pointi 13 mara baada ya kushinda michezo minne na kwenda sare mmoja.

Mpaka sasa Simba kwenye kundi hilo hajapoteza mchezo wowote na akiwa ameruhusu bao moja tu.

Katika michezo ya ugenini Simba aliyocheza kwenye Ligi ya Mabingwa msimu huu hajapoteza.

Simba amefanikiwa kuifunga AS Vita nchini Congo na kutoka sare ya bila kufungana na Al Merrreikh kwenye mchezo wao uliochezwa Sudan.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!