Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Simba bado mbili, Yanga yaishusha Azam FC
Michezo

Simba bado mbili, Yanga yaishusha Azam FC

Wachezaji wa timu ya Azam wakiwa katika moja ya michezo yake ya Ligi Kuu Tanzania Bara
Spread the love

MICHEZO nane imechezwa leo kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara, ambapo klabu ya Yanga imefanikiwa kuishusha Azam FC kwenye msimamo baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Ndanda, huku Azam FC wakisubilisha Simba ubingwa baada ya kwenda sare ya bao 1-1 dhidi ya Biashara United. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwa matokeo hayo ya Azam FC dhidi ya Biashara yatailazimu Simba kushinda kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Tanzania Prisons ili waweze kutangaza ubingwa.

Mtibwa Sugar ameendelea kupata wakati mgumu baada ya kukubalia kipigo cha bao 1-0, dhidi ya Mwadui huku Namungo akilazimishwa sare ya bao 1-1, dhidi ya Ruvu Shooting.

Matokeo mengine ya michezo ya leo Alliance imepata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union, Singida amekubali kichapo cha mabao 3-2 akiwa nyumbani mbele ya Lipuli Fc.

KMC wamelazimishwa sare ya bao 1-1 na Kagera Sugar kwenye Dimba la Kaitaba na Mbeya City ameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Jkt Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!