Tuesday , 16 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Silinde achukua fomu Tunduma, atuma salamu Chadema
Habari za Siasa

Silinde achukua fomu Tunduma, atuma salamu Chadema

Spread the love

ALIYEKUWA mbunge wa Momba kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), DAVID Silinde amechukua fomu ya kugombea ubunge Tunduma Mkoa wa Songwe kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Silinde amechukua fomu hizo leo Jumanne tarehe 14 Julai 2020. Hadi mchana, wagombea 16 walikuwa wamekwisha chukua fomu kuwania nafasi hiyo.

Jimbo la Tunduma lilikuwa linaongozwa na Mbunge wa Frank Mwakajoka wa Chadema.

Soma zaidi hapa

David Silinde ajiuzulu

MwanaHALISI Online limezungumza na Silinde ambaye amesema, “nimepokelewa vizuri na uongozi wa wilaya na kupewa fomu” huku akisema Chadema hakiwezi kushinda Tunduma katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020.

“Mimi kama mwanachama mpya, nitafuata taratibu zote kulingana na katiba, kanuni na mwongozo na ikiwa nitapitishwa au mtu yoyote kati yetu atapitishwa tutamuunga mkono,” amesema Silinde

“Tutaendesha kampeni za kistaarabu. Sisi kama chama tumejiandaa kushinda Tunduma na sioni kama Chadema wakishinda,” amesema Silinde ambaye amekuwa mbunge kwa miaka kumi mfululizo

 

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia amfariji mjane wa Musa Abdulrahman

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne amempa pole Mwanakheri Mussa...

Habari za Siasa

Nape: Wanasiasa, wanahabari, wafanyabiashara mteteeni Samia

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,...

Habari za Siasa

CAG: TAWA imegawa vibali vya uwindaji bila idhini ya waziri

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

Habari za Siasa

TAMISEMI yatenga bil. 17.79 kwa ajili uchaguzi serikali za mitaa

Spread the loveWIZARA Ofisi ya Rais-TAMISEMI, imetenga fedha kiasi cha Sh. 17.79...

error: Content is protected !!