Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Silaha za kivita zakutwa kwenye gari lililomteka Mo
Habari Mchanganyiko

Silaha za kivita zakutwa kwenye gari lililomteka Mo

Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro amesema silaha ya kivita aina ya AK-47, pisto tatu pamoja na risasi 19 zimekutwa katika gari lililotumika kumteka Mfanyabiashara Mohammed Dewji ‘Mo Dewji’. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 20 Oktoba 2018, IGP Sirro amesema polisi baada ya kufanya ukaguzi ndani ya gari hilo aina ya Toyota Surf ambalo lilitelekezwa usiku wa kumkia leo na wanaodaiwa kumteka Mo Dewji, wamekuta silaha hizo hatari.

IGP Sirro ameeleza kuwa, kutokana na hatari ya silaha hizo, watekaji hao kama wangefanikiwa  kutoroka na Mo Dewji nje ya nchi ingekuwa hatari zaidi.

“Katika upekuzi ndani ya gari tumekuta sialaha nne, silaha ya kivita na kuna uwezekano wametoka nayo kwao na pisto tatu. Baada ya kufanya ukaguzi Mohamed alitekwa kwa silaha nne, ni hatari sana na kama wangetoroka naye ingekuwa shida sana, risasi 19 za kivita na silaha ambazo unaweza piga mfululizo,” amesema IGP Sirro.

IGP Sirro amesema watekaji hao  baada ya kuona kwamba hawawezi kutoroka nje ya nchi kutokana na uwepo wa ulinzi mkali, waliamua kuliterekeza gari hilo. Na kwamba kama wangechelewa kidogo Jeshi la Polisi lingewakamata.

“…Hii gari imetelekezwa hapa Mo akawa ameachiwa lakini ameeleza kwamba watu hawa walikuwa wanahitaji fedha, fedha kiasi gani hawakusema, lakini anasema walikuwa na wasi wasi sana, wanahoji wakiwa na wasi wasi wakiwa na silaha zao.

Walipotoka Colosseum walikwenda moja kwa moja kumpeleka chumbani,  aliwapa simu ya baba yake wazungumze nae lakini kwa sababu ulinzi wetu ulikuwa imara wakawa wanaogopa  kuwasiliana na wazazi wake,” amesema IGP Sirro.

Katika hatua nyingine, IGP Sirro amesema Jeshi la Polisi limebaini mtandao uliohusika kumteka Mo Dewji ambao wahusika wametoroka kurudi nchini mwao.

Mo Dewji mfanyabiashara maarufu ndani na nje ya nchi ambaye pia ni muwekezaji katika klabu ya Simba, alitekwa alfajiri tarehe 11 Oktoba katika hoteli ya Colosseum iliyoko maeneo ya Oesterbay  jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!