Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Shule za msingi zakabiliwa upungufu walimu 100,958
Elimu

Shule za msingi zakabiliwa upungufu walimu 100,958

Wanafunzi wa shule ya msingi
Spread the love

 

SHULE za Msingi nchini zinakabiliwa na upungufu wa walimu 100,958 kwa kuangalia uwiano wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 60. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hayo yamebainishwa leo Alhamisi tarehe 14 Aprili katika hotuba ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI iliyowasilishwa bungeni na Waziri Innocent Bashungwa.

Katika hotuba hiyo Bashungwa amesema takwimu zilizopo zinaonesha kuwa kuna jumla ya Shule za Msingi 17,034 zenye jumla ya wanafunzi 12,033,594 wakiwemo wanafunzi wenye mahitaji maalum 60,825.

Waziri wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Innocent Bashungwa

Amesema hadi Machi, 2022 mahitaji ya walimu katika Shule za Msingi ni 274,549 kwa kutumia uwiano wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 60 huku walimu waliopo ni 173,591.

“Upungufu ni walimu 100,958 sawa na asimilia 36.77 ya mahitaji,” amesema Bashungwa.

Aidha, amesema mahitaji ya walimu kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum kwa Shule za Msingi ni ni walimu 3,631, waliopo ni 1,517 na upungufu ni walimu 2,143 sawa na asilimia 59.02 ya mahitaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!