Tuesday , 21 March 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Shule ya Kandwi Z’bar yapata neema
Elimu

Shule ya Kandwi Z’bar yapata neema

Spread the love

 

BENKI ya Exim imetoa Sh.10 milioni kwa taasisi ya Asma Mwinyi Foundation (AMF), kwa ajili ya kuwezesha ununuzi wa vifaa vya ujenzi na ukarabati vyoo vya shule ya awali, msingi na sekondari ya Kandwi, Unguja, visiwani Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Stanley Kafu, amesema, wanatambua changamoto za elimu visiwani hivyo, “tumejitolea kuhudumia watu, biashara na jamii kwa ujumla.”

“Tunafurahi kuwa sehemu ya mkakati huu muhimu unaolenga kuinua mazingira ya elimu Zanzibar. Tunaona taasisi ya AMF kuwa mshirika sahihi katika kufanikisha dhamira hiyo,” amesema Kafu

Alisema, wana dhamira inayofanana kati ya benki hiyo na AMF ya kusaidia juhudi za kielimu na ustawi wa wanafunzi na shule kote nchini.

“Wanafunzi hutumia muda mwingi zaidi katika siku wakiwa shuleni hivyo ni muhimu zaidi tukiweka jitihada katika kuboresha mazingira ya vyoo vyao,” alisema.

Naye Asma, aliishukuru benki hiyo huku akibainisha kuwa, msaada huo utagusa maisha ya wanafunzi wengi kwa miaka mengi ijayo.

“Wadau wetu muhimu na washirika kama Benki ya Exim, ndio nguzo muhimu kwa mafanikio yetu. Tunashukuru kwa msaada huu ambao utasaidia katika kukarabati vyoo vya shule ya awali, msingi na sekondari ya Kandwi,” alisema

Wawakilishi wa shule hizo, Kheir Juma Pandu na Juma Haji Ame walisema, kukamilika kwa ujenzi na ukarabati wa vyoo hivyo kutasaidia kuhudumia wanafunzi zaidi 700 waliopo katika shule hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Elimu

Mfuko wa Jimbo Musoma Vijijini wamwaga mamilioni ujenzi maabara za sekondari

Spread the love  MFUKO wa Jimbo la Musoma Vijijini, Mkoa wa Mara,...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

Elimu

Harambee ujenzi sekondari za Musoma Vijijini yashika kasi

Spread the love  HARAMBEE ya ujenzi na ukarabati wa shule za sekondari...

Elimu

Shule ya Alpha yazindua mfumo wa kugundua vipaji vya watoto

Spread the love  SHULE ya Sekondari ya Alpha ya jijini Dar es...

error: Content is protected !!