Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Shule ya Alpha yazindua mfumo wa kugundua vipaji vya watoto
Elimu

Shule ya Alpha yazindua mfumo wa kugundua vipaji vya watoto

Mratibu wa Mtaala wa ziada wa Shule ya Sekondari ya Alpha, Fulgence Kabiligi
Spread the love

 

SHULE ya Sekondari ya Alpha ya jijini Dar es Salaam imezindua mfumo wa kupima na kugundua vipaji vya watoto kidigitali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mfumo huo utahusika kupima vipaji vya watoto kijidigitali ili kuweza kusaidia watoto kuendelezwa katika vipaji vyao na kuvitumikia ipasavyo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mfumo huo Profesa wa Sheria na mtoa mihadhara maarufu kutoka nchini Kenya, Patrick Lumumba, alisema watasambaza ujumbe huo mzuri kuwa shule za Alpha ndio zimechaguliwa kuwa kitovu anzilishi cha mfumo huo mpya ambao utakuwa na manufaa kwa vijana wa kike na wakiume wa kitanzania na Afrika pia.

Prof Lumumba alieleza kuwa kupitia mfumo huo vijana watakaotambuliwa vipaji vyao watawezeshwa ili mafanikio yao yasikwazwe bali yapewe rutuba.

“Kupitia mfumo huu mtoto atapimwa kipaji chake na kusaidiwa kukitumia vizuri. Kila mtu ana kipaji ila wengine hawajui hivyo kushindwa kuvitumia ipasavyo,”alisisitiza Prof Lumumba.

Kwa upande wake Mratibu wa Mtaala wa ziada wa shule ya Alpha, Fulgence Kabiligi, alisema hata kabla ya ujio wa mashine hiyo, shule yao ilijikita kugundua vipaji kwa kuanzisha vilabu 21 na kufundisha jinsi ya kuwa wajasiriamali.

“Hii mashine ni kwa ajili ya Watanzania wote kwani itagundua watoto wenye uwezo mkubwa, mdogo na ambao hawana watatafutiwa utaratibu.

Alisema manufaa yake inamsaidia kupima kipaji na kukijua na kuendelezwa katika shule ya kipaji husika na kusoma kwa haraka na muda mfupi ili kuweza kutumia kipaji chake.

“Mtoto anapimwa na mwanasaikolojia kujua historia yake, asili na anapendelea nini baadae anaingia kwenye mashine inachukua vina saba na wanatoa michoro ambayo inatumwa mtandaoni wanasoma na kurudisha majibu ndani ya dakika chache,”alieleza Kabaligi.

Alifafanua kuwa watakuwa na kliniki zitakazoendeleza vipaji, vyuoni na watashirikiana na shirikisho la vipaji duniani na kupima vipaji na wakigundulika watachukuliwa kwenda nje kwa lengo la kuendelezwa.

Alifafanua kuwa mashine hiyo ni kamera ya kawaida haina mionzi wala madhara kwa binadamu.

“Tutaweka uratibu wa kupima kwa watu ambao hawana uwezo tutatumia serikali za mitaa na tutatumia pia utaratibu taratibu za shirikisho la vipaji duniani na kliniki zitakuwa na gharama kidogo tutashirikiana na serikali,”alisisitiza.

Naye Afisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, Abdul Maulid, alisema ikiwa watoto watapimwa kupitia mfumo huo itarahisisha kwani wapo wazazi wanawalazimisha watoto kusoma mambo ambayo hawana uwezo nayo.

Alisema wao wanatumia waalimu kugundua vipaji vya watoto kutokana na elimu walizopatiwa kwa muda mrefu.

“Tulikuwa tunajua kuwa huyu mwanafunzi anafaa kusoma sayansi, biashara au sanaa kwa kumfuatilia ufaulu wake, ila mfumo huo utaondoa shida kwa mzazi kutaka mtoto wake kuwa kama yeye atafata kipaji chake,”alisisitiza.

1 Comment

  • @THINK/Dedication/Remember”@ EMPLOY/US THEM ALL – ALL TANZANIAN HAS JOB TO DO

    In 2021, the unemployment rate in Tanzania remained nearly unchanged at around 2.74 percent. With a decline of 0.04 percentage points, there is no significant change to 2020. Over the observed period, the unemployment rate has been subject to fluctuation.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

Elimu

Takukuru wambana Mwalimu mkuu, atema bungo

Spread the loveMwalimu Mkuu wa shule msingi Hanihani, kata ya Igunga wilayani...

error: Content is protected !!