SHIRIKA la kimataifa la kutetea haki za binadamu, Amnesty International limeitaka Jeshi la Polisi kumpa dhamana au kumfikisha mahakamani, Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe anayesota rumande tangu juzi tarehe 31 Oktoba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Zitto anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam baada ya kukamatwa akiwa nyumbani kwake maeneo ya Masaki, akidaiwa kutoa taarifa za uongo kuhusu mauaji ya baadhi ya askari polisi na wananchi katika kijiji cha Mpeta wilayani Uvinza mkoa wa Kigoma.
Amnesty limetoa wito huo kupitia akaunti yake ya Twitter, ambapo limeitaka vyombo vya dola kumfungulia mashtaka mahakamani Zitto au kumuacha huru mara moja.
Wakati akizungumza na wabahari katika ofisi za ACT zilizoko Kijitonyama jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba 2018, Zitto alidai kuwa wananchi zaidi ya 100 wamepoteza maisha katika vurugu zilizoibuka kutokana na mgogoro wa ardhi wilayani Uvinza, taarifa iliyopingwa vikali na Jeshi la Polisi mkoani Kigoma.
Kabla ya Zitto kukamatwa na Polisi, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Kigoma, Martin Ottieno alimtaka Zitto kuwasilisha vielelezo vya madai yake kuwa yametokea mauaji ya watu 100 mkoani humo, ikiwemo makaburi.
The authorities in #Tanzania have detained opposition party leader @ZittoKabwe without charge for speaking out against recent killings in his constituency. @tanpol should charge him with a recognizable crime or release him immediately and unconditionally. #FreeZittoKabwe pic.twitter.com/WMNZc5Njis
— Amnesty Eastern Africa (@AmnestyEARO) November 1, 2018
Leave a comment