Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Shirika la Kimataifa laingilia kati kukamatwa kwa Zitto
Habari za SiasaTangulizi

Shirika la Kimataifa laingilia kati kukamatwa kwa Zitto

Spread the love

SHIRIKA la kimataifa la kutetea haki za binadamu, Amnesty International limeitaka Jeshi la Polisi kumpa dhamana au kumfikisha mahakamani, Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe anayesota rumande tangu juzi tarehe 31 Oktoba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Zitto anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam baada ya kukamatwa akiwa nyumbani kwake maeneo ya Masaki, akidaiwa kutoa taarifa za uongo kuhusu mauaji ya baadhi ya askari polisi na wananchi katika kijiji cha Mpeta wilayani Uvinza mkoa wa Kigoma.

Amnesty limetoa wito huo kupitia akaunti yake ya Twitter, ambapo limeitaka vyombo vya dola kumfungulia mashtaka mahakamani Zitto au kumuacha huru mara moja.

Wakati akizungumza na wabahari katika ofisi za ACT zilizoko Kijitonyama jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba 2018, Zitto alidai kuwa wananchi zaidi ya 100 wamepoteza maisha katika vurugu zilizoibuka kutokana na mgogoro wa ardhi wilayani Uvinza, taarifa iliyopingwa vikali na Jeshi la Polisi mkoani Kigoma.

Kabla ya Zitto kukamatwa na Polisi, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Kigoma, Martin Ottieno alimtaka Zitto kuwasilisha vielelezo vya madai yake kuwa yametokea mauaji ya watu 100 mkoani humo, ikiwemo makaburi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!