Saturday , 2 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Shibuda wa tatu kuteuliwa kugombea urais Tanzania
Habari za Siasa

Shibuda wa tatu kuteuliwa kugombea urais Tanzania

Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemteua John Shibuda wa Ada Tadea kuwa mgombea urais wa Tanzania na Hassan Konde Kijongoo  kuwa mgombea mwenza katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Uteuzi wa wagombea hao umefanywa leo Jumanne tarehe 25 Agosti 2020 na Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Semistocles Kaijage.

Jaji Kaijage amefanya uteuzi huo baada ya kujiridhisha Shibuda na Kijogoo wamedhi vigezo.

Shubuda amekuwa mgombea wa tatu kuteuliwa na NEC akitanguliwa na Rais John Pombe Magufuli wa Chgama Cha Mapinduzi (CCM).

           Soma zaidi:-

Wa pili kuteuliwa ni Leopard Mahona wa NRA kuwa mgombea urais wa Tanzania na Ally Khamis Hassan kuwa mgombea mwenza.

Vyama vilivyochukua fomu kuwania kuteuliwa kugombea urais ni 17 kati ya 19 vyenye usajiliwa kudumu.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa na habari mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia kuzindua programu ya nishati safi ya kupikia kwa wanawake Afrika

Spread the loveRais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua programu ya...

Habari za Siasa

AG aiagiza kamati ya maadili kuwashughulikia mawakili wanaokiuka maadili

Spread the loveMWANASHERIA Mkuu wa Serikali (AG), Dk. Eliezer Feleshi, ameagiza Kamati...

Habari za Siasa

Jaji avunja ukimya sakata la Mpoki kusimamishwa uwakili

Spread the loveJAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, amekitaka Chama cha...

Habari za Siasa

Sheikh Ponda ataka mwarobaini changamoto uchaguzi 2020

Spread the loveKATIBU Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa...

error: Content is protected !!