Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Sheria ya bima ya ajali ipitiwe upya – Spika Tulia
Afya

Sheria ya bima ya ajali ipitiwe upya – Spika Tulia

Spread the love

SPIKA wa Bunge la Jamhuri, Dk. Tulia Ackson Mwansasu, ameitaka serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bima (TIRA), kuangalia upya utaratibu wa mashirika ya bima kuwalipa waathirika wa ajali nchini. Anaripoti Maria David … (endelea).

Alisema, kuna umuhimu wa kuwekwa utaratibu wa kisheria wa kuyalazimisha makapuni ya bima kulipa wahanga kwa haraka na sharti muda huo uelezwe kwenye sheria.

Dk. Tulia alitoa kauli hiyo, kwenye semina kuhusu usalama barabarani iliyoandaliwa kwa ajili ya wabunge na wizara ya mambo ya ndani ya nchi, iliyofanyika bungeni jijini Dodoma.  

Alisema Bunge liko tayari kusaidia kurekebishwa kwa sheria ya bima, iwapo itabainika kuwa ni muhimu kufanya hivyo.

Alisema, “…huwa sifurahi sana watu kusumbuliwa mahakamani, kwa mfano gari imeanguka na watu wamefariki au wamejeruhiwa sasa hawa watu wanahusika vipi na uzembe wa dereva.”

Alihoji, “kwanini bima zisiwalipe waathirika kwanza kisha ikaendelea na mambo mengine ya mahakamani kwa huyo mfanyabiashara?”

Akaongeza, “watu wa TIRA tusaidieni katika hilo na kama ni changamoto za kisheria sisi mtuletee tuifanyie kazi na haya yote ni lazima tubadili mtazamo; tunatamani haya mambo kuyatazama kwa upana sana.”

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

AfyaTangulizi

Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli

Spread the loveTIMU ya wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Amsterdam cha nchini...

Afya

Wananchi 530,000 kufaidika na ujenzi wa hospitali ya bil. 1.8

Spread the love  SERIKALI imetoa Sh 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi...

error: Content is protected !!