Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Sheria Maudhui ya Mtandao kukatiwa rufaa
Habari Mchanganyiko

Sheria Maudhui ya Mtandao kukatiwa rufaa

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

MAHAKAMA Kuu, Kanda ya Mtwara leo tarehe 12 Juni 2019, imetoa kibali cha kukata rufaa ya kupinga Kanuni za Maudhui ya Mtandao ya Mwaka 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Baraza la Babari Tanzania (MCT), Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Muungano wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu kwa pamoja waliomba kibali cha kukata rufaa mahakama hiyo kupinga matumizi mapya ya mtandao.

Katika kesi hiyo namba 25 ya mwaka 2018 ilifunguliwa na wadau hao wa habari, washtakiwa ni Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Mwanasheria Mkuu.

Akisoma hukumu katika Shauri la Maombi No. 5 la 2019 mbele ya Wakili Humphrey Mtuy, anayewakilisha jopo la mawakili wa waleta maombi na Wakili Wilbroad Ndunguru, akiwakilisha mawakili wa serikali, Jaji Dkt. Fauz Twaib amesema kuwa, pande zote mbili zimeonesha kutokuridhishwa na matumizi ya neno maudhui ingawa wamekuwa na hoja tofauti.

Na kwamba, maombi hayo yanahusisha watumiaji wengi wa mitandao walioathirika na uamuzi ya mwanzo wa kutumika kwa kanuni hizo.

Jajai Twalib ameridhia kuwa, maombi ya rufaa yapelekwe katika Mahakama ya Juu (Mahakama ya Rufaa) kwa ajili ya kusikilizwa na kutolewa uamuzi.

Awali, Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mtwara ilitupilia mbali shauri la kupinga matumizi ya kanuni za maudhui ya kimtandao.

Hukumu hiyo ilitolewa tarehe 9 Januari 2019 na Jaji Wilfread Ndyansobera. Jaji huyo alisema kuwa, maombi hayo hayakuwa na uzito.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

error: Content is protected !!